|
Unataka kuchangia lolote kuhusiana na yaliyomo kwenye tovuti hii? Au una lolote lingine ambalo ungependa kulisema ili kubadilishana mawazo na wasomaji wengine wa tovuti hii? Huu ni ukurasa wako mahsusi kwa ajili hiyo tuandikie feedback@chezasalama.com
| WANAWAKE MNATUUA UA! |
Karibia kila kiungo cha mwanamke kinavutia na kusisimua! Kuanzia nywele, macho, mdomo, shingo, mabega, chuchu, tumbo, kiuno, hipsi, makalio, mapaja, miguu, sura, sauti, tembea na kila kitu! Hivyo, kama tunataka kuumaliza UKIMWI basi wanawake acheni kufanya visa vya makusudi! Punguzeni kulegeza sauti, kurembua macho, mapozi na kutingisha makalio mnapotembea, kuvaa nguo fupi za kubana na zenye mipasuo, acheni kazi ya u-stejishoo, kujiremba na kupaka wanja, kula ovyo na kuwa na makalio makubwa na mahipsi. Punguzeni kuwa na miili iliyolegea kama mlenda...mkifanya yote haya tutautokomeza UKIMWI. Bila ya hivyo wanaume tutazidi kudata na UKIMWI hautakwisha.
Loverboy
born4sex@beautifulboy.com |
|
| TAARIFA ZENU VIJIJINI JE? |
Vijana wengi wana elimu isiyo sahihi au hawana kabisa elimu ya afya na UKIMWI. Tovuti yenu inatusaidia kwa kiasi kikubwa kutuelimisha juu ya hilo, na tunafurahi sana kuona kuwa mnaijali jamii. Lakini, elimu hii haiwafikii sana watu wa vijijini ambako hakuna mtandao. Mawazo yangu ni kuwa ni vyema kama likianzishwa gazeti la AFYA BOMBA ambalo litasambazwa hadi vijijini ili wapate taarifa kuhusu afya zao na wajifunze mambo mbalimbali ya maisha.
Sharbano
sharbanoabubakar@hotmail.com |
|
| WASICHANA JIFUNZENI KUSEMA ‘NO’ |
Nawashauri vijana hasa wasichana wajifunze kusema "NO" kwa wanaume wanaowadanganya kwa hela. Ni kweli kwamba maisha yana ugumu lakini, watafute shughuli ndogondogo waweze kujipatia mahitaji yao ya kila siku ili wasiwe tegemezi.
libeseba1@hotmail.com |
|
| TUFUATE AMRI ZA MUNGU |
Maoni yangu ni kwamba ili gonjwa hili tulitokomeze, TUFUATE AMRI ZOTE ZA MUNGU NA TUZIDISHE UCHA MUNGU ILI TUKAPUMZIKE MAHALIPEMA . AMIN.
msagatt60@yahoo.com |
|
| NIMEACHIKA SABABU YA MAWASILIANO |
Ngoja niwaeleze wenzangu kuhusiana jinsi nilivyoachika ile nao wajifunze. Mimi nilikuwa bize sana kwenye shughuli zangu, simu sina, kwake siendi hadi mawasiliano yakapungua kwa kiasi kikubwa. Sasa mwenzangu naye hakuwa mwaminifu hivyo akatafuta msichana mwingine ambaye ni mpangaji mwenzake. Siku nilivyokwenda kumtembelea mwenzangu, nikakuta mabadiliko. Sikuwa na jinsi ila nikajua ni makosa yangu pamoja nae pia. Hivyo napenda kutoa ushauri wenye wapenzi mawasiliano ni bora kwa kuwa yanawafanya mnakuwa pamoja ile kimawazo tu.
vero_mwanga@yahoo.com |
|
| MSIFANYE NGONO BILA KUPIMA |
Naomba watu waache kufanya ngono bila kupima wawe waminifu. Pia kujua afya zetu ni vizuri zaidi.
marycamara2004@yahoo.com |
|
| NIMEJIFUNZA MENGI CHEZASALAMA |
Tovuti hii ni nzuri sana tena inaelimisha sana. Mpaka sasa mimi binafsi nimejifunza mengi sana kutokana na tovuti hii naomba waendelee kutuelimisha na pia wasikate tamaa.
graceroman2003@yahoo.com |
|
|