Logo
Sera ya Lugha kiengerezi

Chagua Lugha
Kuingia katika majadiliano

 
   
   Hujaandikishwa?
   Andikisha
hapa

   Homepage > Habari na Burudani > Sauti yako
Sauti yako

Unataka kuchangia lolote kuhusiana na yaliyomo kwenye tovuti hii? Au una lolote lingine ambalo ungependa kulisema ili kubadilishana mawazo na wasomaji wengine wa tovuti hii? Huu ni ukurasa wako mahsusi kwa ajili hiyo tuandikie feedback@chezasalama.com

WANAWAKE MNATUUA UA!
Karibia kila kiungo cha mwanamke kinavutia na kusisimua! Kuanzia
nywele, macho, mdomo, shingo, mabega, chuchu, tumbo, kiuno, hipsi, makalio, mapaja, miguu, sura, sauti, tembea na kila kitu! Hivyo, kama tunataka kuumaliza UKIMWI basi wanawake acheni kufanya visa vya makusudi! Punguzeni kulegeza sauti, kurembua macho, mapozi na kutingisha makalio mnapotembea, kuvaa nguo fupi za kubana na zenye mipasuo, acheni kazi ya u-stejishoo, kujiremba na kupaka wanja, kula ovyo na kuwa na makalio makubwa na mahipsi. Punguzeni kuwa na miili iliyolegea kama
mlenda...mkifanya yote haya tutautokomeza UKIMWI. Bila ya hivyo wanaume tutazidi
kudata na UKIMWI hautakwisha.

Loverboy
born4sex@beautifulboy.com
TAARIFA ZENU VIJIJINI JE?
Vijana wengi wana elimu isiyo sahihi au hawana kabisa elimu ya afya na UKIMWI. Tovuti yenu inatusaidia kwa kiasi kikubwa kutuelimisha juu ya hilo, na tunafurahi sana kuona kuwa mnaijali jamii. Lakini, elimu hii haiwafikii sana watu wa vijijini ambako hakuna mtandao. Mawazo yangu ni kuwa ni vyema kama likianzishwa gazeti la AFYA BOMBA ambalo litasambazwa hadi vijijini ili wapate taarifa kuhusu afya zao na wajifunze mambo mbalimbali ya maisha.

Sharbano
sharbanoabubakar@hotmail.com
WASICHANA JIFUNZENI KUSEMA ‘NO’
Nawashauri vijana hasa wasichana wajifunze kusema "NO" kwa wanaume wanaowadanganya kwa hela. Ni kweli kwamba maisha yana ugumu lakini, watafute shughuli ndogondogo waweze kujipatia mahitaji yao ya kila siku ili wasiwe tegemezi.
libeseba1@hotmail.com
TUFUATE AMRI ZA MUNGU
Maoni yangu ni kwamba ili gonjwa hili tulitokomeze, TUFUATE AMRI ZOTE ZA MUNGU NA TUZIDISHE UCHA MUNGU ILI TUKAPUMZIKE MAHALIPEMA . AMIN.
msagatt60@yahoo.com
NIMEACHIKA SABABU YA MAWASILIANO
Ngoja niwaeleze wenzangu kuhusiana jinsi nilivyoachika ile nao wajifunze. Mimi nilikuwa bize sana kwenye shughuli zangu, simu sina, kwake siendi hadi mawasiliano yakapungua kwa kiasi kikubwa. Sasa mwenzangu naye hakuwa mwaminifu hivyo akatafuta msichana mwingine ambaye ni mpangaji mwenzake. Siku nilivyokwenda kumtembelea mwenzangu, nikakuta mabadiliko. Sikuwa na jinsi ila nikajua ni makosa yangu pamoja nae pia. Hivyo napenda kutoa ushauri wenye wapenzi mawasiliano ni bora kwa kuwa yanawafanya mnakuwa pamoja ile kimawazo tu.
vero_mwanga@yahoo.com
MSIFANYE NGONO BILA KUPIMA
Naomba watu waache kufanya ngono bila kupima wawe waminifu. Pia kujua afya zetu ni vizuri zaidi.
marycamara2004@yahoo.com
NIMEJIFUNZA MENGI CHEZASALAMA
Tovuti hii ni nzuri sana tena inaelimisha sana. Mpaka sasa mimi binafsi nimejifunza mengi sana kutokana na tovuti hii naomba waendelee kutuelimisha na pia wasikate tamaa.
graceroman2003@yahoo.com