|
Vipi, unataka kushtukizwa au kupitwa na matukio? Je unataka watu wengine wawe taarifa zaidi kuliko wewe? Hakika jibu ni HAPANA! Sehemu hii itakupa habari zote za nini kinachotarajiwa kufanyika ili uweze kwenda na wakati! Iwe habari nzito nzito au mambo ya burudani ikiwa pamoja na michezo, usanii na mitindo. Kwa ajili ya haya na mengine mengi 'itembelee' sehemu hii uhabarike!
Maonyesho
7th Jan 08 to 31st Jan 08
at Wasanii Centre, Slipway
Wasanii wane kuonyesha sanaa zao za uchoraji. Wasanii hao ni Saidi Mbaraki, David Mzuguno, Omari Kanyaki na Fadhil Omari
Sanaa ya Cuba leo
14th Jan 08 to 31st Jan 08
at Alliance Francaise, Dar es Salaam
Kundi la wasanii wakali wa Cuba kufanya maonyesho yake
Usiku wa tamaduni mchanganyiko
16th Jan 08
at Alliance Francaise, Dar es Salaam
Furahia Machifu Band (reggae), Fujo, Dancsi na Mionzi Dance Theatre, Fanani Flava Poetry Club, Rasta Agon Acrobatics, Jam Session, Muziki wa video na mziki mchanganyiko wa Kiafrika na DJ Alliance
Mkutano wa Fema
21st Jan 08 to 23rd Jan 08
at Silver sands, Dar es Salaam
Femina HIP kuwa na mkutano wa taifa kuhusu Uongozi wa Vijana kuhusu Elimu ya VVU/UKIMWI na Ujinsia mashuleni
Mashindano ya baiskeli
3rd Feb 08
at Dar es Salaam
Washiriki zaidi ya 30 kuwania ubingwa wa taifa wa baiskeli
Ngumi za vijana
15th Feb 08
at Dar es Salaam
Mashindano ya ngumi za vijana wenye umri chini ya miaka 20
Bingwa wa ndondi za ridhaa
27th Mar 08 to 2nd Apr 08
at Mlimani Park Mwenge, Dar es Salaam
Mashindano ya kumsaka bingwa wa ndondi za ridhaa. Klabu zaidi ya 20 kushiriki
Dar Mwenyeji wa Mwenge wa Olympik
13th Apr 08 to 14th Apr 08
at Dar es Salaam
Kutokana na historia yake ya amani, Dar es Salaam imechaguliwa kuwa jiji pekee la Afrika, ambapo Mwenge wa Uhuru utapita na kusimama ukielekea Beijing, China.
Mkutano wa nane wa Sullivan
2nd Jun 08 to 6th Jun 08
at Arusha
Mkutano wa Leon H. Sullivan kuwajumuisha viongozi wa dunia wa kisiasa, kibiashara, mashirika yasiyo ya kiserikali (ya kimataifa na kitaifa), taasisi za taaluma kwa ajili ya kuzungumzia maendeleo ya kiuchumi vya Afrika. Maudhui ya mkutano huo ni “Maendeleo ya Utalii na Miundombinu.
|