Chagua swali hapa chini kuona jibu lake!
|
Kama umeshaambukizwa na ukianza kutumia dawa za kurefusha maisha utaishi kwa muda gani zaidi? |
|
Kwanini wajane huishi muda mrefu sana baada ya waume zao kufa kwa UKIMWI? |
|
Je, tuwatenge waliokwishaambukizwa virusi vya UKIMWI? |
|
Kama mwathirika anaweza kuishi miaka mingi, kwanini matangazo kuhusu UKIMWI hutilia kifo msisitizo? |
|
Kwanini serikali isiwatenge waathirika ili wasiendelee kuambukiza wengine? |
|
Kwanini serikali isiwatangaze hadharani waliokufa kwa UKIMWI? |
Kama umeshaambukizwa na ukianza kutumia dawa za kurefusha maisha utaishi kwa muda gani zaidi?
Muda utakaoongezeka unatofautiana kati ya mtu na mtu kuendana na:
-Hali ya mtu wakati anaanza matibabu -Uwezo wa kufuata masharti ambayo ni: -Kutumia dawa kwa kufuata ratiba bila kukosa -Kujitunza, kula kwa kufuata kanuni za afya -Kuwahi kutibiwa magonjwa nyemelezi mapema
|
Kwanini wajane huishi muda mrefu sana baada ya waume zao kufa kwa UKIMWI?
Muda wa kuishi tangu kuathirika unatofautiana kati ya mtu na mtu. Wako wanaoishi muda mfupi, kiasi au mrefu kutokana na mambo kadha wa kadha kama vile lishe bora, kujitunza, kutibiwa maradhi na kujijali katika mambo yote ya kimwili. Yawezekana wajane hawa wakaishi muda mrefu kwa kuzifuata kanuni bora za kuishi na VVU.
|
Je, tuwatenge waliokwishaambukizwa virusi vya UKIMWI?
Watu wenye UKIMWI ni binadamu na wana haki kama binadamu wengine. Watu hawa wanahitaji misaada na mawazo yetu. Mila na desturi zetu tangu awali hazitengi watu wenye matatizo kiafya bali huwatunza na kuwapa msaada. Hivyo, kuwatenga watu wenye UKIMWI ni ishara ya kuvunja familia na kuleta taabu nyingi katika jamii.
Pia kitendo hicho, kitalipunguzia taifa letu nguvu kazi yenye kutegemewa kwa kuwa baadhi ya watu wenye UKIMWI bado ni hazina kwani wana utaalamu katika nyanja mbalimbali. Vilevile, bado wanahitajika katika familia zao n.k.
|
Kama mwathirika anaweza kuishi miaka mingi, kwanini matangazo kuhusu UKIMWI hutilia kifo msisitizo?
Ni bahati mbaya, kampeni nyingi husisitizia kwamba anayeathirika hufa. Kampeni za namna hii huimarisha unyanyapaa. Ni vema matangazo haya yakaonyesha pande zote mbili, yaani waathirika wenye afya nzuri na waathirika wenye hali isiyo ya kuridhisha
|
Kwanini serikali isiwatenge waathirika ili wasiendelee kuambukiza wengine?
Haki za binadamu za kimataifa na kitaifa zinawalinda waathirika na familia zao na serikali haiwezi kuingilia kati. •Wasinyanyapaliwe wala kutengwa. •Hata hivyo nani atengwe na nani asitengwe? •Tungelipima wote na kuwa wazi bado tungeendelea kuishi pamoja.
Kuwatenga waathirika siyo njia sahihi ya kuzuia usambazaji wa VVU Jambo la msingi ni kutoa elimu ya kutosha ili wasieneze VVU.
|
Kwanini serikali isiwatangaze hadharani waliokufa kwa UKIMWI?
Haki za binadamu zinawalinda hata waliokufa. Hasara za kutangaza ni kubwa kuliko faida za kutangaza. Hata kama serikali ingetangaza, watakaopata taarifa ni wale waliopo kwenye mazishi. Yawezekana matangazo haya yasifike kule walikopatia maambukizi/alipokuwa anaishi. Na tujiulize matangazo haya yatamsaidia nani saa hizi?
La msingi ni kuwa elimu ya kutosha itolewa, hakuna haja ya kutangaza. Jilinde na uwalinde wengine.
|